Thursday, November 22, 2007

Ngosha anapotoka na Ngosha!


Baada ya kupumzika kwa muda kidogooo na kudeal na shughuli zake binafsi,Farid Kubanda (Fid Q) mwenye maskani yake mkoani Mwanza anajiandaa kutoka tena kwa kishindo kikubwa kama kawaida yake hapo mapema mwezi Dec.Kutoka kwa Fid safari hii kutakuwa tofauti kwani anajiandaa kurelease kwa mpigo track yake mpya iitwayo 'Ngosha' kwenye vituo vya radio..sambamba na video.Track hiyo imepangwa kutoka Jumamosi ya tarehe 15 Dec,na itakuwa ni moja ya kazi za utambulisho wa albam yake ya pili inayotarajiwa kutoka hapo mwakani.

No comments: